Sunday 22 June 2014

Wapiganaji wa jihad waiteka miji zaid


Wapiganaji wa ISIS
Wapiganaji wa Jihadi wameendelea kuyateka maeneo zaidi nchini Iraq,baada ya kuliteka eneo moja la kivuko karibu na mpaka wa Syria, na sasa wanalekea mjini Baghdad kupitia bonde la Euphrates.
Mwandishi wa BBC nchini Iraq amesema kuwa hatua hiyo inawafungulia njia wapiganaji wengine wa ISIS nchini Syria.
Wapiganaji hao vilevile wameiteka miji zaidi katika mkoa wa Anbar ambapo mwandishi huyo anasema kuwa lengo lao ni kuitumia kuvamia mji mkuu wa Baghdad.
Waasi hao wanasema kuwa waliiteka miji hiyo bila kumwaga damu kupitia majadiliano na makabila ya kisunni.
Wanamgambo wa Kishia hapo jana walifanya gwaride mjini Baghdad, na kuzua wasiwasi kuhusu tofauti inayozidi kuibuka kati ya watu wa dhehebu la kishia na wale wa Kisuni.

No comments: