Sunday 22 June 2014

Ghana yatoshana nguvu na Ujerumani

Ujerumani 2-2 Ghana
Asamoah Gyan aliifungia Ghana bao la pili na kusadia Black Stars kusajili alama yake ya kwanza katika kombe la dunia baada ya kuambulia kichapo cha 2-1 dhidi ya Marekani katika mechi yao ya kwanza.
Baada ya kipindi cha kwanza kuishia sare tasa, nipe nikupe baina ya timu hizo zilizaa matunda dakika tano baada ya kipindi cha pili kuanza.
Mario Gotze alikuwa ameifungia Ujerumani bao la kwanza kwa kichwa kunako dakika ya 51 lakini furaha yao haikudumu kwani Andre ayew akaisawazishia Black stars dakika tatu tu baadaye.
Matumaini ya timu ya Afrika kufuzu kwa mkondo wa pili yaliimarika Nahodha Asamoah Gyan alipoiweka Ghana mbele kunako dakika ya 63 ya kipindi cha pili.
Bara la Afrika lilihuzunishwa Miroslav Klose alipofuma kona ya Ujerumani kimiani na kuisawazishia ujerumani kunako dakika ya 71 ya mechi hiyo na hivyo timu hizo zikagawanya alama mechi ilipokamila mabao yakiwa ni 2-2 .
Kufuatia bao hilo la Klose mjerumani huyo anayeicheza Lazio ameweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika historia ya kombe la dunia kwa pamoja na Ronaldo.
klose amefunga mjumla ya mabao 15.
Ujerumani 2-2 Ghana
Kwa upande wake Asamoa Gyan naye ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kutoka barani Afrika ambaye amefunga mabao katika michuano tatu ya kombe la dunia.
Vijana wa Joachim Low sasa wamejikita kileleni mwa kundi G wakiwa na alama 4 moja zaidi ya Marekani huku Ghana ikiwa ya tatu na alama moja kutokana na sare hii ya leo.
Ureno licha ya kuwa na wachezaji wenye haiba ya juu kama vile Christiano Ronaldo bado wanaburuta mkia wakiwa bila ya alama yeyote .
Black stars sasa watakuwa wanaomba kuwa Christiano Ronaldo ataisaidia Ureno kuibana Marekani kisha nao wailaze Ureno iliwafuzu kwa mkondo wa pili.

No comments: