Saturday 7 June 2014

Waasi watumia watoto kama wanajeshi wao Sudani



Zaidi ya watoto 9,000 wamekuwa wakitumiwa kama wanajeshi katika vita vivayoendelea nchini Sudan Kusini.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa mkuu wa haki za binadamu katika umoja wa Mataifa Navi Pillay.
Pande zote kwenye mgogoro huu , wanajeshi na waasi wamedaiwa kuwasajili watoto kupigana.
Bi Pillay amesema kuwa Sudan Kusini inakabiliwa na tisho la njaa , lakini viongozi wake hawaonekani kuliona hilo kama swala muhimu la kushughulikiwa.
Alikuwa anazungumza mwishoni mwa ziara yake nchini Sudan Kusini ambako mgogoro wa wenyewe kwa wenyewe umewaacha mamiioni ya watu bila makao.
Vita vilizuka mwezi Disemba kati ya wanajeshi wa serikali wanaomtii Rais Salva Kiir na hasimu wake kiongozi wa waasi, Riek Machar ambaye anatuhumiwa kwa kuanzisha mgogoro huu kwa kuwa na njama ya kumuondoa mamlakani.
Riek Machar pia wakati mmoja alikuwa makamu wa Rais wa Salva Kiir.
Machar amekanusha madai hayo lakini amekuwa akiongoza waasi wanaopigana dhidi ya serikali.
Pande zote mbili zimekuwa kwenye meza ya mazungumzo kujaribu kusitisha vita lakini hakuna mabadiliko katika hali inayokumba nchi hiyo, Vita vingali vinaendelea.

No comments: