Thursday 26 June 2014

Australia yatangaza eneo jipya la kuisaka ndege ya Malaysia

Ndege ya Malaysia ikiitafuta meli iliyoweka
Ndege ya Malaysia ikiitafuta meli iliyoweka

Serikali ya Australia imetangaza eneo jipya la kuitafuta ndege ya abiria ya Malaysia iliyotoweka na zaidi ya abiria 200 mwezi Machi mwaka huu.

Naibu Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Warren Truss amesema baada ya wataalam kuthathmini upya ni wapi ndege hiyo inawezakuwa iliangukia, eneo hilo jipya ni Kilomita 1,800 Pwani Magharibi wa Australia.
Ndege hiyo ya abiria MH370 ilitoweka ghafla ikielekea jijini Beijing nchini China ikitokea jijini Kuala Lumpur nchini Malaysia ikiwa na abiria 239 wengi wao wakiwa raia wa China.
Wataalam wanasema kuwa baada ya uchunguzi wao wamebaini kuwa ndege hiyo ilikuwa haindeshwi na rubani ilipozama.
Ripoti ya serikali ya Australia yenye ukurasa 64 imependekeza kuwa utafutaji huo ufanyika katika eneo la Kilomita 60,000 mraba.
Meli maalum ya Marekani ikiitafuta ndege ya Malaysia
Mwezi Aprili, Mataifa ya Magharibi yakiongozwa na Marekani yalituma meli maalum za majini kujaribu kuitafuta ndege hiyo sakafuni mwa bahari bila mafanikio.

Utafutaji wa ndege hii ndio ghali zaidi katika historia ya utafutaji wa ndege ya abiria iliyopotea katika mazingira ya kutatanisha. Familia za abiria waliotoweka baada ya kupotea kwa ndege hiyo wanasema wameghabishwa na kutopatikana kwa mabaki ya ndege hiyo ambayo hadi sasa haijulikani ilipo.

No comments: