Monday 11 May 2015

Bob junior na diamond kupiga kolabo hivi karibuni

BAADA ya kushangaza wengi alipohudhuria katika sherehe ya Zari All White Party iliyoandaliwa na msanii Abdul Nasib ‘Diamond’ anayedaiwa kutoelewana naye, prodyuza Raheem Rummy ‘Bob Junior’, ameendelea kushangaza wengi kwa madai kwamba wapo mbioni kurekodi wimbo wa pamoja na msanii huyo.
Prodyuza huyo aliweka wazi mipango yake hiyo huku akidai tayari ameshanunua baadhi ya vifaa vipya kwa ajili ya kuimarisha studio yake iwe katika ubora wa kimataifa kama studio nyingine zinazoongoza kwa ubora duniani.
“Hiyo ni zaidi ya ‘surprise’, kwa ubora wa vyombo vyangu nina imani ‘beat’ itakayotoka hapo itakuwa kwenye kiwango cha hali ya juu na kazi yetu itakuwa nzuri sana,” alimaliza.

No comments: