Wednesday 13 May 2015

Ngasa mchezaji rasmi wa Free state ya Afrika kusini

Mrisho Ngassa akimiliki mpira
Sasa ni rasmi, mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa amemwaga wino kuichezea klabu ya Free State Stars ya Ligi Kuu Afrika Kusini kwa miaka minne .
Ngasa ameripotiwa kufurahia mkataba huo mnono na kuanza kwake kwa maisha mapya baada ya kucheza nyumbani kwa miaka kadhaa.
Ngasa ameonekana katika mitandao kadhaa akiwa na kocha wa timu hiyo baada ya kusaini mkataba.
“Nataka kutumia fursa hii kuitangaza soka ya Tanzania na nitajituma ili kufanya vizuri zaidi", amesema mchezaji huyo.

No comments: