Raia huyo wa Ufaransa alimpa Renaud Prudhomme,
mwenye umri wa miaka 56, ''shoti'' 56 za mvinyo katika baa yake
Raia
huyo wa Ufaransa alimpa Renaud Prudhomme, mwenye umri wa miaka 56,
''shoti'' 56 za mvinyo katika baa yake kwa nia ya kuvunja rekodi ya
mywaji pombe nambari moja.Marehemu Prudhomme, aliyekuwa ameandamana na binti yake kujiburudisha, alipelekwa nyumbani akiwa mlevi chakari.
Inaarifiwa kuwa alikimbizwa hospitalini ambapo alipatikana ameaga dunia siku iliyofuatia.
Hata hivyo mahakama ilimpata na hatia mhudumu huyo Gilles Crepin, mwenye umri wa miaka 47, kwa kumchochea marehemu Prudhomme aendelee kubugia mvinyo ilihali alikuwa mlevi kupindukia.
Mahakama ilisema kuwa Crepin aliendelea kuandika nani anayeshikilia rekodi hiyo kwenye ubao uliotundikwa hadharani kwa wateja wake.
Sasa Crepin amehukumiwa kifungo cha nyumbani cha miezi minne na kupigwa marufuku ya kufanya kazi katika baa yeyote kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Wakili wake Renaud Portejoie tayari amesema kuwa atakata rufaa dhidi ya kauli hiyo ya mahakama.
Awali alikuwa ameiambia mahakama kuwa kifo cha Prudhomme hakikutokea kimsingi na kufuatia matukio ya mteja wake kwani marehemu alikuwa na maradhi ya kupumua mbali na kuwa mraibu wa tembo.
''kwa hakika hatuwezi kuwalazimisha wateja wote wa pombe kutoa ithibati kuwa wako katika hali nzuri ya afya''
Wakili wa mwanawe marehemu Antoine Portal, alisema kuwa familia yao imetulizwa na marufuku hiyo ya Crepin ya mwaka mmoja.
''Nilikuwa nataka tu kuwakumbusha wahudumu wa baa kuwa ni kinyume cha sheria kuendelea kumpa pombe mlevi''
No comments:
Post a Comment