Sunday 31 May 2015

Pierre Nkurunziza akataa kuhudhuria kikao kitakachozungumzia nchi yake

Rais Nkurunziza
Msemaji wa rais wa Burundi amesema kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza hatahudhuria mkutano wa viongozi wa kikanda ambao utaangazia mzozo ulio nchini mwake.
Msemaji huyo aliliambia shirika moja la habari la Ufaransa kuwa rais Pierre Nkurunziza atakuwa akifanya kampeni ya uchaguzi wa urais na kwamba waziri wa mashauri ya kigeni ndiye atahudhuria mkutano ambao utawajumuisha marais wa Rwanda, Uganda , Tanzania na Kenya mjini Dar es Salaam.
Wakati Nkurunziza alihudhuria mkutano kama huo mpema mwezi huu baadhi ya maafisa wa kijeshi walijaribu kumpindua.
Burundi imekumbwa na ghasia tangu Nkurunziza atangaze kuwa atawania urais kwa muhula wa tatu.
Hapo jana Nia ya rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu ilipata pigo baada Afisa mmoja tume hiyo ya uchaguzi kuiambia redio moja ya Ufaransa kuwa Spes Caritas Ndironkeye aliabiri ndege ijumaa na haijulikani kama alijiuzulu au la.
Maafisa wa Polisi wanalaumiwa kwa kusababisha vifo vya waandamanji 20
Tume hiyo ya uchaguzi ina maafisa wakuu watano na inaweza kuendelea kuhudumu hata baada ya kuondoka kwa mmoja wao.
Hata hivyo duru zinaelezea kuwa huenda afisa wa pili wa tume hiyo akajiondoa na hivyo kulemaza shughuli za tume hiyo.
Juma lililopita kanisa katoliki nchini Burundi lilijiondoa kutoka kwa harakati zozote za uchaguzi mkuu uliokumbwa na utata siku moja tu kabla ya umoja wa Ulaya kuondoa maafisa wake katika shughuli hizo za uchaguzi.
Umoja wa ulaya ulikuwa umetuma maafisa wa kucimamia na kuhakikisha kuwa uchaguzi huo ni wa huru na haki.
Taarifa hiyo imetokea wakati ikisalia wiki moja tu uchaguzi wa wabunge na madiwani ufanyike nchini humo.
Maandamano dhidi muhula wa tatu wa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza yanaendelea kufanyika katika mitaa kadhaa ya mji mkuu Bujumbura
Kanisa katoliki ni kiungo muhimu katika suala la amani na demokrasia nchini Burundi tokea kuanzishwa mazungumzo ya amani ya Arusha mnamo miaka ya tisini.
Haya yamearifiwa wakati maandamano dhidi muhula wa tatu wa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza yanaendelea kufanyika katika mitaa kadhaa ya mji mkuu Bujumbura kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.
Makundi ya kutetea haki za binadamu, yanasema kuwa zaidi ya watu 20 wamefariki wakati wa ghasia za maandamano,
Tangu rais Pierre Nkurunziza alipotangaza mwezi uliopita kuwa anapania kuwania tena kiti cha urais kwa muhula wa tatu, kinyume na katiba ya Burundi.
Uchaguzi wa urais umepangiwa kufanyika Juni tarehe tano, huku ule wa urais ukiwa mwishoni mwa mwezi huo wa Juni.

No comments: