Saturday 23 May 2015

Marekani yasimamisha kwa muda mafunzo ya kijeshi kwa wanajeshi wa Burundi

Msemaji wa wizara ya mambo ya nchi za nje wa Marekani Marie Harf, amesema nchi hiyo imesimamisha kwa muda mafunzo inayotoa kwa wanajeshi wa Burundi kwa ajili ya operesheni za kulinda amani, kutokana na wasiwasi kuwa mgogoro wa kisiasa nchini Burundi huenda ukaathiri uwezo wa wanajeshi wake wa kushiriki katika operesheni hizo. Uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza mwezi uliopita wa kutaka kuwania muhula wa tatu madarakani, umesababisha maandamano yaliojaa vurugu, jaribio la kuipindua serikali na kusababisha maelfu ya warundi kukimbilia nchi jirani. Kulingana na Ikulu ya Marekani tangu mwaka wa 2005 kupitia mpango wa kutoa mafunzo na kuwasaidia wanajeshi wa Africa ACOTA, Marekani imeshatoa mafunzo hayo kwa wanajeshi wa kulinda amani  zaidi  ya 248,000 katika nchi 25 barani Afrika kabla ya kupelekwa katika kikosi cha Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika katika operesheni za kulinda amani.

No comments: