Saturday, 23 May 2015
Waziri Mkuu wa togo ajiuzulu pamoja na serikali yake
Waziri Mkuu wa Togo Kwesi Seleagodji Ahoomey-Zunu na serikali yake walijiuzulu hapo jana Ijumaa, hatua iliotarajiwa baada ya Rais wa nchi hiyo Faure Gnassingbe kushinda uchaguzi mwezi uliopita na hivyo kuendeleza takriban miaka 50 ya utawala wa familia yake. Tarehe nne mwezi huu, rais Gnassingbe aliapishwa rasmi kuchukua uongozi wa muhula wake wa nne baada ya kushinda kwa asilimia 59 ya kura katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi. Aidha rais Gnassingbe alimshukuru Waziri Mkuu na serikali yake kwa kuitumikia nchi akikubali kwamba kujiuzulu kwao kunaendana na utaratibu wa nchi hiyo. Hata hivyo haijawa wazi iwapo baadhi ya mawaziri waliojiuzulu watapewa nyadhifa za uongozi katika serikali mpya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment