Mabaki ya ndege yaliyopatikana kweye ufukwe wa kisiwa cha Reunion
katika Bahari ya Hindi siku ya Jumatano huwenda yakawa ni shemu ya bawa
la ndege ya shirika la ndege la Malaysia Airlines iliyotoweka mwaka
mmoja uliyopita kulingana na maafisa wa Malaysia na Australia.
Kugunduliwa kwa chombo hicho, ambacho kimethibitishwa na waatalamu
kua ni kutoka ndege ya aina ya Boieng 777, imesababisha kuanzishwa
uchunguzi mpya kutafuta ndege ya shirika la Malaysia MH370 iliyotoweka
Marchi 8 2014, ilipokuwa safarini kutoka Kulalumpar kuelekea Bejing.
Watu
watatu wamelazwa katika hospitali teule ya Shirati wilayani Rorya baada
ya kujeruhiwa vibaya katika ugomvi ambao unadaiwa kuhusishwa na kampeni
za kisiasa za wagombea wa ubunge wa chama cha mapindizikatika jimbo la
Rorya mkoani Mara.
Mmoja wa majeruhi wa tukio hilo, amesema walishambuliwa na chupa
huku wakitishiwa kukatwa mapanga muda mfupi baada ya kumalizika mkutano
wa kampeni za CCM katika eneo hilo.
Siku
moja baada ya mbunge wa Monduli Edward Lowassa kujiunga na Chadema
baadhi ya wasomi nchini wamempongeza kwa ujasili aliouonyesha.
Kabla ya kujiunga na Chadema, wadadi wa masuala ya siasa za Afrika
wanasema ni Tanzania na Zimbabwe pekee ndizo zilizokuwa bado
hazijatikishwa kisiasa, lakini kwa Tanzania Julai 28 bado itakumbukwa.
AZAM FC jana ilimaliza ubabe wa Yanga katika michuano ya Kombe la
Kagame baada ya kuibuka na ushindi wa penalti 5-4 katika mchezo wa robo
fainali uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Timu hizo zilifikia hatua ya kupigiana penalti baada ya kutoka suluhu
katika dakika 90 za kawaida za mchezo huo, uliokuwa wa vuta nikuvute
katika kipindi chote.
Haji Mwinyi ndiye aliyeitia Yanga doa baada ya kukosa penalti ya
tatu, huku Azam FC ikipata penalti zote tano. Waliofunga kwa upande wa
Azam FC ni Kipre Tchetche, John Bocco, Humid Mao, Pascal Wawa na Aggrey
Morris wakati walioifungia Yanga ni Salum Telela, Nadir Haroub na
Godfrey Mwashiuya.
Haroub alikosa penalti katika mchezo dhidi ya Gor Mahia ya Kenya
wakati Yanga ikilala 2-1, huku Simon Msuva na Amis Tambwe wakikosa
penalti zao katika mchezo dhidi ya Telecom ya Djibouti, licha ya timu
yao kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 katika hatua ya makundi.
Kwa ushindi huo, Azam FC sasa watakutana na KCCA katika mchezo wa
nusu fainali utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa kesho, huku Gor Mahia
ikicheza dhidi ya Khartoum ya Sudan katika mchezo utakaotangulia wa nusu
fainali.
Nguli
wa soka Duniani ,Diego Maradona amemtuhumu mke wake wa zamani Claudia
Villafañe kwamba kumuibia kiasi cha fedha zipatazo dola milioni tisa,
katika akaunti yake ya benki.
Akizungumza katika matangazo ya moja
kwa moja ya Luninga,Maradonna amesema Villafañe ambaye alikuwa mpenzi
wake wa zamani ni mwizi. Hata hivyo Villafañe amepinga vikali madai na
kudai kuwa yeye si mwizi na hakuiba fedha hizo.
Dakika chache baada ya kutangaza kutangaza kujiunga rasmi na UKAWA
kupitia Chadema, waandishi wakamuuliza kuhusu Sakata la RICHMOND....
Sikia alivyojibu hapa kwenye hii Video:
Msemaji
wa rais wa Nigeria,Muhammadu Buhari,amesema amejipanga kupambana na
kundi la kigaidi la Boko Haram kama litaendesha mashambulizi yake katika
mipaka ya kimataifa.
Msemaji huyo , Garba Shehu , aliiambia BBC
kuwa tangu rais Buharia chaguliwe mwezi Mei amejipanga kutatua migogoro
inayoikabili nchi hiyo tangu wananchi wa Nigeria wampa dhamana ya
kuwaongoza.
MAPADRI watatu na mtawa mmoja wa Kanisa Katoliki Jimbo la Rulenge
wilayani Ngara walifariki dunia jana papo hapo huku watu 13 wakijeruhiwa
katika ajali ya barabarani wakiwahi Karagwe kwenye misa ya shukrani ya
mwenzao aliyepata daraja hilo hivi karibuni.
Tukio lingine ni la juzi ambapo watu saba walikufa na wengine 44
kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha basi na treni ya mizigo mkoani
Tabora. Ajali hiyo ya juzi watu wanne walikufa papo hapo huku wengine
wakifia njiani wakipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora, Kitete.
Katika tukio la kwanza la Ngara, kwa mujibu wa mmoja wa mapadri
waliokuwa katika msafara huo, Erasto Nakule, ajali hiyo ilitokea jana
saa 2:00 asubuhi katika barabara iendayo nchi jirani ya Uganda katika
eneo la Bugorora wilayani Missenyi mkoani Kagera.
Alisema gari aina ya Land Cruser lenye namba ya usajili T.650 BY1 la
Jimbo Katoliki la Rulenge lililokuwa likiendeshwa na Padri Florian
Tuombe ambaye pia amefia katika Hospitali ya Mkoa Kagera liligongana uso
kwa uso na basi la Kampuni ya Sabuni lenye namna ya usajili T.166 AGU.
Watu
wanne wamefariki papo hapo na wengine zaidi ya arobaini kujeruhiwa
baada ya Treini ya mizigo,kuligonga basi kampuni ya Don’t Worry
lililokuwa likitokea mjiniTabora kuelekea ufuruma uyui mkoani humo
lilipofika eneo la kuvuko cha reli eneo loa malolo manispaa ya Tabora
katika kile kilichodaiwa kuwa ni uzembe wa dereva.
Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa, dereva aliyekuwa katika
mwendo wa kasi alitaka kukatiza haraka bila kuzingatia eneo hilo
inapopita Treini hata kama aliiona Treini hiyo, na ndipo alipokata kona
ya ghafla na basi hilo kuanguka kwenye reli na Treini kuigonga na
kukutoa paa lote la juu la gari.
Tatizo
la mashine kutokutambua alama za vidole limejitokeza kwa baadhi ya
vituo wakati zoezi la uandikishaji likiendelea jijini Dar es Salaam na
kusababisha mashine kuzima zaidi ya mara sita huku tatizo la ubovu wa
mashine na waandikishaji wasiokuwa na uzoefu likiendelea kulalamikiwa.
Licha ya kuwepo kwa malalamiko tangu siku ya kwanza ya zoezi hili
kuanza hapa jijini lakini mamlaka husika zimeonekana kushindwa kuyatatua
kwa wakati hali inayopelekea msongamano kwa baadhi ya vituo
kutokupungua na watu kulazimika kuamka usiku wa manane kuwahi namba za
uandikishwaji siku moja kabla.
TanzaniaOne blog imetembelea vituo mbalimbali na kushuhudia wananchi wakiwa
wamejipumzisha vivulini na wengine wakichapa usingizi wakisubiri kuitwa
majina huku kina mama wenye watoto wakilalamikia kutokupewa kipaumbele.
Baadhi ya waandikishaji waliozungumza na Ukomboz Blog wamedai kuwa tatizo la
vidole vya baadhi ya wananchi kutokusoma kwenye mashine limekuwa
likijitokeza mara kwa mara na kulazimika kutumia muda mwingi kuhudumia
mtu mmoja hali inayozua kelele kwa watu waliopo kwenye foleni.
Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Temeke akizungumzia zoezi hilo
amesema changamoto ambayo wamekuwa wakikabiliana nayo mara kwa mara ni
watu kupiga simu vituoni hasa wanapoona wenzao hawafuati utaratibu na
kuongeza kuwa hakuna aliyeshikiliwa kutokana na vurugu zinazojitokeza
katika vituo hivyo.
Wakati
vuguvugu la uchaguzi mkuu wa rais,wabunge na madiwani likiendelea kwa
kasi mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha demokrasi na mendeleo
chadema Bi.Chiku Abwao amejitoa katika chama hicho na kujiunga rasmi na
chama cha ACT wazalendo.
Bi.Abwao amesema ameridhishwa na uongozi wa ACT-wazalendo, katiba
na ilani ya uchaguzi wa chama hicho hadi kumpelekea kuamua kujiunga kwa
vile kinalenga kumkomboa mtanzania masikini pamoja na kuweka msingi
imara ya maadili ya viongozi.
SASA ni rasmi kuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa anajiunga
katika Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na leo anatarajiwa
kuzungumzia suala hilo, lililotanda katika siasa za Tanzania tangu baada
ya kutopata nafasi ya kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa
mgombea wake wa urais.
Msemaji wake, Aboubakary Liongo alithibitisha jana jioni kuwa mbunge
huyo wa Monduli, atazungumza saa 10 kamili jioni leo Dar es Salaam,
kutoa kauli yake kuhusu mwaliko wa Ukawa, umoja ulioasisiwa wakati wa
mchakato wa Bunge Maalumu la Katiba mwaka jana, ukimwalika ajiunge nao.
Liongo alieleza kuhusu mkutano huo wa leo, baada ya wakuu wa vyama
vinavyounda Ukawa kuzungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi Kuu za
Chama cha Wananchi (CUF), Buguruni, Dar es Salaam na kuchukua fursa hiyo
kumwalika Lowassa kujiunga nao na kumsafishia njia ya kuwa mgombea wao
wa urais.
“Tunachukua fursa hii kipekee kumwalika Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge
wa Jimbo la Monduli, Mheshimiwa Edward Lowassa ajiunge na Ukawa na tuko
tayari kushirikiana naye katika kuhakikisha tunaiondoa CCM madarakani
katika Uchaguzi Mkuu ujao. “Tunaamini Mheshimiwa Lowassa ana uwezo wa
kuhamasisha umma kuikataa CCM yenye kusimamia mifumo isiyotenda haki. Ni
mchapakazi makini na mfuatiliaji wa karibu wa utendaji katika majukumu
anayokabidhiwa,” alisema Mwenyekiti wa Taifa wa NCCR-Mageuzi, James
Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa Ukawa wakati akisoma taarifa
ya Ukawa.
Watu
saba wamenusurika kifo baada ya kula chakula kinachodaiwa kuwa na sumu
kwenye tafrija ya maulidi ya kumtoa mtoto nje katika eneo la Nkuhungu
manispaa ya Dodoma.
Watu hao mara baada ya kula chakula hicho ambacho kilikuwa ni
kitoweo cha nyama ya mbuzi mikate na asali walianza kutapika mfululizo
kabla ya wasamaria wema kuwakimbiza hosipitali ya rufaa ya mkoa wa
Dodoma ambapo muuguzi mfawizi wa hosipitali hiyo Rehema Mghina
akithibitisha kupokea watu hao huku akisema kuwa bado wako kwenye
utafiti wa kitabibu ili kugundua wagonjwa hao wanasumbuliwa na tatizo
gani.
Viongozi
wa Vyama vinavyunda Umoja wa vyama vya Upinzani Tanzania (UKAWA) wakiwa
katika Ofisi za Makao makuu ya Chama cha CUF, katika Mkutano na
waandishi wa Habari mapema leo.
Na. Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Mwenyekiti
mwenza, ndugu James Mbatia ndie alikuwa wa kwanza kuongea. Ni rai ya
UKAWA kwa kila mtanzania ambae yuko tayari kuondoa mfumo kandamizi wa
CCM kuungana nasi. Tunachukua fursa hii kumualika waziri mkuu mstaafu na
mbunge wa Monduli kujiunga na UKAWA. Ni mchapakazi makini na
mtekelezaji wa majukumu, UKAWA ndio tumaini la Tanzania, tusikubali
kunyamaza pale ambapo sauti zetu zinazimwa kwa lazima. Mungu ibariki
Tanzania, Mungu ibariki UKAWA, UKAWA ndio tumaini letu.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kulia) akifurahia jambo na wajumbe
wa Kamati Kuu ya chama hicho walipohudhuria kikao cha dharura katika
Hoteli ya Bahari Beach, jijini Dar es Salaam jana. kuanzia kushoto ni
Ezekia Wenje, Mchungaji Peter Msigwa na Naibu Katibu wa chama hicho
(Zanzibar), Salum Mwalimu.
Licha ya Baraza Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF)
kupokea taarifa ya Ukawa na kuamua chama hicho kiendelee kushiriki
katika umoja huo, bado suala la mgombea urais wa vyama vinavyounda umoja
huo limeendelea kuwa siri nzito.
Taarifa
zilizopatikana kutoka ndani ya CUF jana, zilisema kuwa katika kikao
chake kilichoketi juzi na jana mjini Zanzibar, baraza hilo lilipokea
taarifa ya Ukawa, kuithibitisha na kuamua chama hicho kiendelee na
ushirikiano huo.
Mkutano wa waandishi wafutwa
Pamoja
na hayo, jana kutwa nzima viongozi wa Ukawa walikuwa kwenye vikao
mfululizo na hakukuwa na taarifa rasmi zilizopatikana na hata mkutano na
waandishi wa habari ulioitishwa jana jioni uliahirishwa bila kueleza
utaitishwa tena lini.
Ingawa taarifa ya mkutano wa
Ukawa na wanahabari haikutaja ajenda, habari zilizoenea katika mitandao
ya kijamii zilibainisha kuwa walikuwa wanakusudia ama kutangaza chama
kilichopitishwa na Ukawa kusimamisha mgombea urais au kutangaza jina la
mgombea mwenyewe pamoja na mgombea mwenza.
Vyanzo
mbalimbali ndani ya Ukawa, vilieleza kuwa ufunguo wa hatua hiyo ulikuwa
unashikiliwa na CUF, ambayo hivi karibuni ilijitenga na umoja huo ili
masuala yake yajadiliwe kwanza na vikao vyake vya maamuzi kabla ya
kurejea kwenye meza ya majadiliano.
Taarifa za uhakika
kutoka katika kikao hicho kilichoketi Zanzibar kwa siku mbili,
zilibainisha kuwa wajumbe waliafikiana kinyume na ilivyotarajiwa kuwa
wangevurugana.
Miongoni mwa mambo ambayo inadaiwa wameafikiana ni kuwa mgombea urais atoke Chadema na chama hicho kitoe mgombea mwenza.
Jussa: Watanzania mtafurahi
Hata
hivyo, mmoja wa wajumbe wa baraza hilo, Jussa Ismail Ladhu alipoulizwa
alisema ikiwa itaamuliwa mgombea mwenza wa Ukawa atoke CUF, hakutakuwa
na shida kwa kuwa chama hicho kina wanasiasa wazuri, safi na makini na
kwamba kitatoa mtu ambaye Watanzania wote watafurahi.
“Ikiamuliwa
kuwa mgombea mwenza atoke CUF, wananchi msiwe na wasiwasi, CUF ina
hazina nyingi, itatoa mtu bora, itawapa chaguo ambalo Watanzania wote
wataridhika nalo,” alisema Jussa.
Pamoja na
kuthibitisha kuwa Baraza hilo limeamua CUF iendelee kushiriki katika
umoja huo, Jussa alisema kwenye mjadala matatizo kidogo yalikuwapo
katika mgawanyo wa majimbo.
Hata hivyo alisema baada ya
kuweka vigezo vya kuwa na mgombea wa Ukawa, sasa hakuna shida kwa kuwa
majimbo machache yaliyosalia utaratibu wake utatangazwa hivi karibuni.
Kuhusu
mgombea mwenza, Jussa alisema CUF ina nafasi kubwa ya kutoa mgombea
huyo kwa sababu ndicho chama chenye nguvu Zanzibar na kina wanasiasa
mahiri na makini.
Wagombea wetu tunataka wawe ni wale
watakaohakikisha kuwa Katiba Mpya inapatikana mara baada ya uchaguzi ili
kuyaweka sawa mambo yanayohitaji kuwekwa sawa.
Hata
hivyo, kwa mujibu wa Katiba, mgombea urais na mgombea mwenza wanapaswa
kutoka chama kimoja, hivyo kama Chadema itamtoa mgombea urais inabidi
pia mgombea mwenza atoke chama hicho.
Habari ambazo bado si rasmi zinasema kuwa mmoja wa viongozi wa CUF anaweza kuhamia Chadema ili kukidhi matakwa hayo ya Katiba.
Mkurugenzi
wa Haki za Binadamu, Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF,
Salim Bimani alisema kuwa mambo katika Ukawa ni mazuri, wapo waliofikiri
kuwa watavurugana, lakini wamekubaliana na sasa Watanzania wasubiri
kupata wagombea safi katika ngazi zote.
Bimani alisema CUF kitaendelea kushirikiana na vyama vingine vya upinzani nchini ili kuhakikisha demokrasia inazidi kukua.
Mbali na Olunga Yanga pia wanamwania kiungo wa mabingwa hao wa Kenya Khalid Auch, ili kuimarisha safu yao ya kiungo mkabaji
KLABU ya Yanga imeongeza nguvu za kumsajili mshambuliaji wa Gor Mahia
ya Kenya Michael Olunga, ili kuziba nafasi ya Mliberia Kpah Sherman,
anayetarajiwa kujiunga na timu ya Mpumalanga Black Aces inayoshiriki
Ligi Kuu nchini Afrika Kusini.
Uongozi wa Yanga kupitia kwa katibu wake Mkuu Dr Joans Tiboroha
amesema wanatarajia kuanza mazungumzo na viongozi wa Gor kuangalia
uwezekano wa kumpata mshambuliaji huyo ambaye ameonyesha uwezo mkubwa
kwnenye michuano ya Kgame inayoendelea Dar es Salaam Tanzania.
“Olunga ni mchezaji mzuri kila mtu analijua hilo na kwakua Sherman
wakati wowote ataondoka tumeona yeye ndiyo mtu sahihi wa kuziba nafasi
yake kwenye kikosi chetu kusaidiana na Donald Ngoma Amissi Tambwe na
Malimi Busungu,”amesema Tiboroha.
Mbali na Olunga Yanga pia wanamwania kiungo wa mabingwa hao wa Kenya
Khalid Auch, ili kuimarisha safu yao ya kiungo mkabaji baada ya Mbuyu
Twite kuonekana kuchoka kutokana na umri mkubwa aliokuwa nao huku pia
klabu yake ya zamani FC Lupopo kuonekana kuisumbua Yanga kutokana na
usajili wake.
Rais Barack Obama wa Marekani hatimaye amefika nchini Ethiopia katika ziara yake ya pili ya nchi za Afrika.
Ni
mara yake ya kwanza tangu aongoze taifa la Marekani akiwa raisi
kuhutubia wanachama hamsini na mbili wa umoja wa Afrika katika makao
makuu yake yaliyoko Addis ababa.Mazungumzo yao yakiwa yamelenga kutafuta
suluhu ya kutokomeza migogoro ya vita za wenyewe kwa wenyewe sudan ya
kusini.
Raisi Obama,aliwasili nchini Ethiopia akiwa anatokea mjini
Nairobi ambako aliwaambia wakenya kuwa amna kikomo cha kile
wanachokihitaji na kusisitiza kwa kutoa angalizo katika athari za
ukabila na rushwa. Tamaduni mbaya kama unyanyasaji wa kijinsia,ndoa za
kulazimishwa ,tohara kwa watoto wa kike na kutopeleka watoto shuleni.
Ni wiki ya mtikisiko. Hivi ndiyo unavyoweza kuelezea hali
itakavyokuwa nchini kutokana na matukio makubwa ya kisiasa
yanayotazamiwa kutokea ndani ya wiki inayoanza leo ambayo yanaweza
kubadili mwelekeo wa siasa za Tanzania.
Hali hiyo
inatokana na vuguvugu la kisiasa linalohusisha viongozi wenye ushawishi
kuhama vyama vyao vya siasa na kutimkia kwenye vyama vingine, ikiwa ni
siku chache kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, mwaka huu.
Ni
wiki ambayo itapambwa na matokeo ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi wa
CUF kilichofanyika jana mjini Zanzibar kuhusu mustakabali wake ndani ya
Ukawa, ikizingatiwa kuwa hivi karibuni chama hicho kiliamua kujiweka
kando ya vikao vya umoja huo hadi vikao vya juu viamue.
Hata
hivyo, habari ambazo gazeti hili limezipata zinasema kuwa uwezekano wa
chama hicho kujitoa ndani ya Ukawa ulikuwa mdogo kutokana na kuogopa
hasira za wananchi wenye matumaini na umoja huo.
Aidha,
kulikuwa na taarifa kuwa kikao cha jana kilikuwa kinaangalia jinsi
watakavyoshiriki katika umoja huo na kwamba kulikuwa na matumaini
makubwa.
Wachezaji wa Azam FC wakipongezana baada ya Kipre Tchetche kuipatia timu yao bao la pili
Timu ya Azam FC ‘wanalambalamba’
leo wametoa dozi ya magoli 5-0 kwa Adama City FC ya Ethiopia kwenye
mashindano ya Kagame Cup ambayo yanazidi kuchanja mbuga jijini Dar es
Samaa mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa.
SIMBA ina malengo mengi ya kuyatekeleza katka msimu mpya wa Ligi
Kuu Bara, lakini kubwa zaidi ni usajili hasa wachezaji wa kigeni ambapo
imeweka majina ya wachezaji watano mezani ambao wapo kwenye mpango huku
ikiwa na nafasi tatu za wazi kwa wachezaji wa aina hiyo.
Simba ina wachezaji wageni wanne ambao wana
uhakika nao tayari, hao ni Simon Sserunkuma, Hamisi Kiiza na Juuko
Murshid ambao wote ni raia wa Uganda.Pia inatarajia kumalizana na Laudit Mavugo raia wa Burundi.
Rais
Jakaya Kikwete akimwapisha Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Ramadhani
Kombwey (kulia) Ikulu Dar es Salaam jana. Mwingine ni Katibu Mkuu
Kiongozi Balozi Ombeni Sefue
RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya utendaji katika Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC), kwa kumteua aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala wa
Tume hiyo, Kailima Kombwey kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni
Sefue, Kombwey ambaye aliapishwa jana jioni, anachukua nafasi ya
aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Mallaba, ambaye ameteuliwa kuwa
Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
Rais Kikwete pia amemteua Jaji Richard Mziray, kuwa Jaji wa Mahakama
ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na majaji wengine
wapya 13 wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
BAADHI ya vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali, waliokuwa
wakiwania nafasi ya kuteuliwa kuwa wabunge wa viti maalumu baada ya
kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu ujao, wamejikuta wakishindwa katika kura za
maoni.
Kura hizo zilizopigwa juzi na wajumbe wa mkutano wa Umoja wa Wanawake
Tanzania (UWT) ngazi za mikoa yote nchini, isipokuwa Mkoa wa Dar es
Salaam, mbali na kuangusha baadhi ya vigogo, pia zimeibua majina mapya
na kuwapa nafasi za juu, zitakazowapa fursa ya kuteuliwa kuwa wabunge wa
Viti Maalumu na hata pengine uwaziri. Washindi wawili wa juu katika
kura hizo katika kila mkoa, ndio walio na nafasi ya kuteuliwa kuwa
wabunge wa viti maalumu, huku wa kwanza akiwa na nafasi nzuri zaidi,
baada ya kupatikana kwa kura za mgombea urais wa CCM.
Miongoni mwa vigogo walioangushwa, yupo Waziri wa zamani wa Maliasili
na Utalii, Shamsha Mwangunga, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia
na Watoto, Dk Pindi Chana na viongozi wa mikoa wa UWT, wakuu wa wilaya
na wabunge kadhaa wa Viti Maalumu wanaomaliza muda wao.
Mkoa wa Njombe
Waziri
wa masuala ya Nje wa Marekani John Kerry amekashifu matokeo ya uchaguzi
ya Burundi yaliyotolewa hapo jana ambapo rais Pierre Nkurunziza
alitangazwa kusajili ushindi mkubwa.
Kerry ametaja uchaguzi huo
kuwa ukiukaji mkubwa wa katiba na kejeli kwa mfumo wa haki huku
akimlaumu rais Pierre Nkurunziza kwa ghasia zilizotokea nchini humo wiki
chache kabla ya kufanyika uchaguzi.
Rais
wa marekani Barack anatarajiwa kuhutubia kongamano la wajasiriamali
akianza rasmi ziara yake katika eneo la afrika masharaki.
Anatarajiwa
kuzungumzia suala la ufisadi ambapo atataka kuwepo kwa jitihada kubwa
za kupambana na ufisadi na pia kuwahutubia wafanyibiahara vijana nchini
Kenya.
YANGA jana ilitinga robo fainali ya Kombe la Kagame baada ya kupata
ushindi wa pili mfululizo kwa kuizamisha KMKM ya Zanzibar kwa mabao 2-0
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo umewafanya mabingwa hao wa Tanzania Bara kufikisha pointi
sita, pointi moja nyuma ya timu mbili za Al Khartoum ya Jamhuri ya
Sudan na Gor Mahia ya Kenya zinazoongoza Kundi A.
Yanga ilianza kwa kufungwa mabao 2-1 na Gor Mahia wiki moja
iliyopita, lakini Jumatano wiki hii ilizinduka na kuichapa Telecom ya
Djibouti mabao 3-0, na hivyo kufufua matumaini ya kusonga mbele.
Kwa matokeo ya jana, Al Khartoum na Gor Mahia ambazo zilitoka sare ya
bao 1-1 katika mechi ya kwanza jana kwenye uwanja huo, zinaungana na
Yanga kucheza robo fainali wakati KMKM imetupwa nje sawa na Telecom.
Rais wa Marekani, Barack Obama amewasili nchini Kenya, huku kukiwa na
ulinzi mkali sana, ikiwa ni mwanzo wa ziara ya siku mbili nchini humo.
Rais Obama alilakiwa na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.
Rais wa Marekani aliepeana mikoni na viongozi wengine wa Kenya na kutia
sain kitabu maalum cha wageni kabla ya kupanda kwenye gari yake.
Mitaa ya Nairobi ilikuwa imepakawa rangi na kusafishwa, mji ulitumia
kila ilichokuwa nacho kwa ajili ya kumkaribisha Obama kwa kile ambacho
wakenya wamekiita “kurejea nyumbani.”
Kutokana
na zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa
kutumia mfumo wa BVR mkoa wa Dar es Salaam kugubikwa na matatizo lukuki
vyama vya siasa na wadau wa siasa wameitaka tume kuongeza mida pamoka na
kuhakikisha kila kituo kina kuwa na mtaalamu wa komputa.
Zoezi hili likiwa limeingia siku ya tatatu jijini hapa huku idadi
kubwa ya watu wakiwa hawajaandikishwa kwa madai ya ubovu wa mashine na
waandikishaji ambao siyo wataalamu kumepelekea vyama hivyo vya siasa na
wadau kuzungunzia hali hiyo kama wanavyoelezea.
10 wafariki, 55 wajeruhiwa kwenye ajali ya basi iliyotokea karibu na mji mkuu wa Tanzania
Watu 10 wameripotiwa kupoteza maisha na wengine 55 kujeruhiwa baada ya basi moja kupoteza mwelekeo na kugonga mti katika eneo la Chamwino lililoko karibu na mji mkuu wa Dodoma nchini Tanzania. Kamanda wa polisi wa eneo la Dodoma David Mnyambugha, alitoa maelezo na kusema kwamba ajali hiyo ilitokea nyakati za jioni wakati basi hilo lilipokuwa likisafiri kutoka Shinyanga kuelekea Dar es Salaam. Kwa mujibu wa maelezo ya Mnyambugha, basi hilo lilipoteza mwelekeo na kugonga mti na kusababisha abiria 8 kupoteza maisha papo hapo.
Bernard Mensah atia saini mkataba wa miaka 6 na kilabu ya Atletico Madrid
Kilabu ya Atletico Madrid kutoka Uhispania imemsajili kiungo wa kati wa Ghana Bernard Mensah kutoka kilabu ya Vitoria Guimaraes.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa mtandaoni kupitia tovuti rasmi ya Atletico Madrid, Mensah alitia saini mkataba wa miaka 6 baada ya makubaliano ya usajili.
huyooo Roma….Golikipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny, 25, anaondoka klabuni hapo kujiunga na Roma kwa mkataba wa mkopo wa mwaka mmoja.
Szczesny
aliruhusiwa na Arsenal kufanya mazungumzo na Roma juu ya maslahi yake,
kwani tayari wanaye Petr Cech aliyesajiliwa kutoka Chelsea na David
Ospina aliyempoka Szczesny namba yake katikati ya msimu uliopita.
Manchester City wanajiandaa ‘kuvunja benki’ kumnasa kiungo mshambuliaji wa Wolfsburg, Kevin de Bruyne, 24.
Mchezaji
huyo ameshawaambia klabuni kwamba anataka kuondoka kwenda kucheza
Etihad. Matajiri hao wa England wanaingiza dau hilo kubwa baada ya wiki
jana tu kumnasa mshambuliaji wa Liverpool, Raheem Sterling kwa pauni
milioni 49.
City wanaaminika kuanza na ofa ya pauni milioni 40
lakini inavyoonekana watapanda hadi pauni milioni 60 kumnasa mchezaji
ambaye Chelsea waliachana naye wakisema hana kiwango, wakamuuza kwa
pauni milioni 18.
Mchuano mwingine mkali unatarajiwa kuwapo katika Jimbo la Bunda Mjini
ambako Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira atavaana na
Mbunge wa Viti Maalumu, Ester Bulaya
Mbunge wa Viti Maalum alihama juzi CCM na kujiunga Chadema,
Ester Bulaya amesema licha ya kuahidiwa vyeo vingi ukiwamo uwaziri na
ukuu wa wilaya ili asihame CCM, aliamua kuviacha ili aweze kuwasaidia
Watanzania wa chini ambao wameonewa na serikali ya chama hicho kwa miaka
50 iliyopita.
Akihutubia katika mkutano wa hadhara
uliofanyikia katika Viwanja vya Stendi ya zamani mjini Bunda jana,
Bulaya alisema wakati chama chake cha zamani kilipogundua mikakati yake
ya kuhamia Chadema, makada wake walimwendea wakimsihi asitoke, bali
abakie ili apatiwe ukuu wa wilaya au uwaziri.
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Mosha Mahona ameuawa na
wananchi baada ya kuwachoma kwa kisu abiria watano waliokuwa kwenye
daladala linalofanya safari zake kati ya Posta na Ubungo Simu 2000.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura alisema jana kuwa tukio
hilo lilitokea juzi saa moja usiku katika eneo la Magomeni Usalama na
Mahona aliuawa kwa kushambuliwa na wananchi baada ya kudhuru abiria
wenzake.
ALIYEKUWA mgombea urais
kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) January Makamba, amefunguka na
kuwataka wananchi wasife moyo kwa yeye kuishia nafasi ya tano kwa vile
muda bado upo na kwamba hivi sasa wafanye kampeni za kufa mtu ili John
Magufuli aliyechaguliwa na chama hicho aweze kushinda na kuingia Ikulu.
Akizungumza kwenye
mkutano maalum wa Umoja wa Wanawake wa CCM wilayani hapa, ulioitishwa
kwa ajili ya kuchagua madiwani wa viti maalum, Makamba aliyeomba tena
kuchaguliwa kuwa mbunge katika jimbo la Bumbuli, alisema kwamba
anawashukuru wote waliokuwa wakimuunga mkono hadi kufikia nafasi hiyo
ambayo haikuwa yake, bali ni ya wananchi wa Lushoto waliomlea na
Watanzania wote.
Bayern Munich yatangaza kuafikiana na Juventus kwa ajili ya usajili wa Vidal
Kiongozi wa kilabu ya Bayern Munich nchini Ujerumani Karl-Heinz Rummenigge, ametangaza kufanya makubaliano na kilabu ya Juventus kwa ajili ya usajili wa kiungo wa kati Arturo Vidal.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa mtandaoni kupitia tovuti rasmi ya Bayern Munich, Rummenigge alithibitisha kuafikiana na Juventus pamoja na Vidal kuhusu usajili wake
Mbunge
mmoja nchini Zimbabwe alizua kizaazaa bungeni pale alitumia chupi za
kina mama kusisitiza hatma ya raia masikini wa nchini hiyo ambao hawana
uwezo wa kununua chupi mpya.
Katika kikao kilichokua kikipeperusha
moja kwa moja kwenye runinga ya taifa, Priscilla Misihairabwi-Mushonga,
wa chama cha upinzani cha Movement for Democratic Change (MDC), alitoa
karatasi ya plastiki iliyokuwa na chupi hiyo. Kisha akamuuliza waziri wa
fedha na sera za serikali kuhusiana na uagizwaji wa chupi kukuu ambayo
anasema ni ya bei nafuu na zinasababisha madhara makubwa kwa afya ya
kina mama.
''Bwana spika hebu tazama hizi chupi ninazo hapa, hizi ni mpya na hugharimu dola mbili kila moja.''
Mbunge huyo Misihairabwi-Mushonga baadaye
alitimuliwa bungeni baada ya kumkabili vikali mbunge wa chama tawala cha
ZANU-PF
''Hizi zilizoko mkono wangu wa kushoto ni mitumba na hugharimu dola moja kwa chupi mbili. alisema mbunge huyo
Akijibu
swali hilo waziri wa fedha Patrick Chinamasa alimtania mbunge huyo
Misihairabwi-Mushonga kutokana na uamuzi wake wa kubeba chupi hizo
bungeni lakini amesema wizara yake inachunguza suala hilo. ''Bwana
Spika, kabla sijajibu swahili hilo, naamini mheshimiwa mbunge
hangelifanya kitendo kama hicho kusisitiza hoja yake'' alisema waziri
huyo wa fedha.
Uchumi wa Zimbabwe umedorora kwa miaka kadhaa iliyopita
Chinamasa amesema
atalishughulikia suala hilo wiki ijayo wakati atakapotoa taarifa rasmi
ya serikali kuhusuiana na sera zake za kiuchumi.
MABINGWA wa Tanzania Bara Yanga, jana walizinduka katika michuano ya
Kombe la Kagame baada ya kuifunga Telecom ya Djibout kwa mabao 3-0
katika mchezo wa Kundi A uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar
es Salaam.
Yanga iliyoanza vibaya mechi za Kundi A kwa kufungwa 2-1 na Gor Mahia
ya Kenya, sasa inaweza kwenda robo fainali iwapo itashinda mechi zijazo
dhidi ya KMKM na Khartoum N ya Sudan.
Katika mchezo huo, uliochezeshwa na mwamuzi Issa Kagabo wa Rwanda
aliyesaidiwa na Lee Okello wa Uganda na Yeatyew Belachew wa Ethiopia,
mabao ya Yanga yalifungwa na wachezaji waliosajiliwa mwaka huu na hadi
mapumziko walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Waziri mkuu Alexis Tsipras hakuwa na njia nyingje ispokua kuwashawishi
wabunge wa Ugiriki kupigia kura mfuko wa pili wa hatua kali za malipo
ziliyotolewa na wakopeshaji.
Usiku wa
Jumatano kuamkia Alhamisi wiki hii, Bunge la Ugiriki limepitisha mfuko
awamu ya pili ya hatua zilizodaiwa na wakopeshaji. Mageuzi haya yanahusu
sheria za kijamii na mabenki.
Mageuzi haya ni sehemu ya masharti ya mwendelezo wa mazungumzo kwa ajili ya mpango wa tatu wa msaada.
Kwa kura 230 za ndio kwa jumla ya kura 300, serikali ya Alexis
Tsipras ilibidi tena kutegemea sauti za upinzani za vyama vya
Conservative (New Democracy), Kisoshalisti cha Pasok na chama cha mrengo
wa kati cha To Potami.
Timu ya livepool imekamilisha
kumsajili rasmi mshambuliaji mwenye asili ya Jamuhuri ya Kidemokrasia wa
kongo Christian Benteke kutoka Aston Villa kwa kitita paundi milion
32.5.
Benteke alikubali mkataba wa muda mrefu na kuwa mchezaji wa pili kununuliwa kwa gharama kubwa huko England.
Baadhi ya wabunge wa Chadema wamezungumzia taarifa zinazosambaa
zikieleza kuwapo mkakati wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa
kuhamia katika chama hicho, wengi wao wakimkaribisha.
Wakati wabunge hao wakikubali kumpokea, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk
Willibrod Slaa amesema wananchi wasubiri mambo yatakapokuwa tayari
badala ya kutegemea mitandao ya kijamii.
“Nitazungumza pale mambo yatakapokuwa sawa, siwezi kuzungumza sasa,
subirini… sasa hivi mambo mengi yanazungumzwa kwenye mitandao,” alisema
Dk Slaa ambaye pia anatajwa kuwa mgombea wa chama hicho ndani ya Ukawa.
Msemaji wa Lowassa, Aboubakary Liongo alipoulizwa kuhusu kuwapo kwa
mpango huo alisema hawezi kulizungumzia hilo kwa kuwa ni suala la mtu
binafsi. Hata hivyo, jitihada za kumpata Lowassa jana hazikufanikiwa
kwani simu yake iliita pasi na kupokewa.
HAPATOSHI! Vita kali ya kugombea ubunge imezuka katika familia ya Mbunge
wa Temeke Abbas Mtemvu kufuatia watoto wake wawili, Lulu na Sitti
Abbasi Mtemvu ambao kwa pamoja wamechukua fomu ya kugombea ubunge viti
maalum kupitia kundi la umoja wa Vijana (UVCCM) Mkoa wa Morogoro.
Jeshi
la Marekani linasema kuwa mmoja viongozi wa kundi la kigaidi la
al-Qaeda, ameuwaua katika shambulio la angani lililotekelezwa na ndege
za kijeshi za Marekani Nchini Syria.
Idara ya ulinzi ya Pentagon
imesema kuwa Muhsin al-Fadhli, alikuwa kinara wa kundi la Khorasan,
lililotumwa na al-Qaeda, kutoka Pakistan hadi nchini Syria.
Dar es Salaam. Baadhi ya wabunge wa Chadema wamezungumzia taarifa
zinazosambaa zikieleza kuwapo mkakati wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward
Lowassa kuhamia katika chama hicho, wengi wao wakimkaribisha.
Wakati wabunge hao wakikubali kumpokea, Katibu Mkuu wa chama hicho,
Dk Willibrod Slaa amesema wananchi wasubiri mambo yatakapokuwa tayari
badala ya kutegemea mitandao ya kijamii.
“Nitazungumza pale mambo yatakapokuwa sawa, siwezi kuzungumza sasa,
subirini… sasa hivi mambo mengi yanazungumzwa kwenye mitandao,” alisema
Dk Slaa ambaye pia anatajwa kuwa mgombea wa chama hicho ndani ya Ukawa.
Msemaji wa Lowassa, Aboubakary Liongo alipoulizwa kuhusu kuwapo kwa
mpango huo alisema hawezi kulizungumzia hilo kwa kuwa ni suala la mtu
binafsi. Hata hivyo, jitihada za kumpata Lowassa jana hazikufanikiwa
kwani simu yake iliita pasi na kupokewa.
Aliyekamatwa na milion 700 Dodoma arudishiwa pesa zake, polisi yasema alikwenda Dodoma kununua nafaka
Jeshi la polisi mkoani Dodoma limekanusha taarifa zilizozagaa kuhusiana
na Raia wa Asia kukamtwa na fedha zaidi ya sh. m.700 kwa madai ya
kuwahonga wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM ili wamchague mmoja kati ya
waliokuwa wanawania nafasi ya Urais
Polisi imesema kuwa uchunguzi
uliofanywa na jeshi la polisi umebaini kuwa hakuna kosa la jinai
lililothibitika licha ya kukutwa na kiasi
hicho cha fedha, tuhuma za rushwa ambazo ndiyo zilikuwa msingi wa
ukamataji wa mtu huyo hazikuthibitika, kwa kuwa hakuna aliyeona
akizigawa fedha hizo wala hakuna aliyedai kushawishiwa au kugawiwa fedha
hizo.
Askofu mstaafu Desmond Tutu amelazwa katika hospitali moja mjini Cape Town Afrika Kusini.
Familia yake inasema kuwa amekuwa akiugua maambukizi yasioisha na kwamba huenda akatoka hospitalini hivi karibuni.
Bwana Tutu alijiuzulu katika maisha ya umma miaka minne iliopita lakini anaendelea kusafiri maeneo mengi.
Amelazwa hosptalini mara kadhaa katika miaka ya hivi karibuni na kutibiwa saratani ya tezi dume kwa mara kadhaa.
Makubaliano yameafikiwa baina ya Iran na mataifa sita yenye nguvu duniani
Baada
ya mazungumzo ya miezi kadhaa makubaliano ya kihistoria yametangazwa
kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran na mataifa 6 makubwa duniani.
Mawaziri
wa mambo ya nje kutoka Iran na mataifa sita zenye nguvu duniani
wanakutana kwa mara ya mwisho huko Vienna baada ya makubaliano rasmi
kutatangazwa katika mkutano na waandishi habari.
Balozi Federica Mogherini, alipotangaza mapatano hayo
Balozi wa maswala ya kigeni wa
bara Ulaya Federica Mogherini, amechapisha mwenye mtandao wake wa
kijamii wa Twitter kuwa makubaliano kuhusiana na mradi wa kinyunklia wa
Iran yameafikiwa.
Bi Mogherini amesema kuwa ni wazi mazungumzo ya
kidiplomasia yanaweza kuleta mabadiliko makubwa ya sera kushinda
makabiliano ya kijeshi ya miongo kadhaa.
Rais wa Iran , Hassan Rouhani, amesema kuwa majadiliano hayo yamekuwa na ufanisi mkubwa