Saturday 17 May 2014

Mlipuko wa bomu waua watu 43 nchini Syria


Mlipuko wa bomu waua watu 43 nchini SyriaWatu 43 wameuawa baada ya bomu kulipuka katika eneo la kaskazini mashariki mwa Syria karibu na mpaka wa Uturuki. Mlipuko huo uliosababishwa na mtu kujilipua garini umetokea karibu na eneo la mpakani la Bab al Salameh pambizoni mwa mji wa Aleppo. Makumi ya watu pia wamejeruhiwa kwenye mlipuko huo.
Katika upande mwingine waasi wa Syria wanaoungwa mkono na nchi za kigeni wameshambulia na kuharibu kaburi la shahaba Uwais al Qarani katika mji wa Raqqa. Mtukufu Uwais bin Qarani alikuwa mfuasi mtiifu wa Imam wa kwanza wa Mashia, Imam Ali bin Abi Twalib (A.S). Makundi ya kitakfiri yenye itikadi za kufurutu ada, yameshambulia na kuharibu maeneo mengi ya kihistoria na Kiislamu nchini Syria katika miaka mitatu iliyopita kutokana na itikadi zao potofu

No comments: