Tuesday 27 May 2014

Wapiganaji 30 wauawa nchini Ukraine

Wapiganaji wanaounga mkono Urusi wakijinadaa kuvamia uwanja wa ndege wa Donetsk
Takriban wapiganaji 30 wanaounga mkono Urusi,wameuawa katika mapigano yaliyozuka katika uwanja wa ndege mjini Donetsk,Mashariki mwa Ukraine.
Mapigano yalizuka baada ya wapiganaji hao waliokuwa wamejihami wakiunga mkono kujitenga kwa mji wa Donetsk kutoka kwa Ukraine
Wapiganaji hao walijaribu kuuteka uwanja huo mnamo siku ya Jumatatu.
Waandishi walio karibu na uwanja huo wanasema walisikia milio ya risasi hata baada ya mashambulizi na ufyatulianaji wa risasi ingawa msemaji wa jeshi alisema kuwa hali ilikuwa imetulia.
Rais mpya Petro Poroshenko aliahidi Jumatatu kuwa operesheni dhidi ya makundi ya kile alichoita magaidi itakamilika baada ya saa chache wala sio miezi.
Mwakilishi wa mji wa Donetsk ambao tayari umejitangza kuwa taifa,  kwa taarifa ya vifo vya watu 30 ni za kweli.
Makabiliano makali katika uwanja wa ndege wa Donetsk
Mmoja wa wapiganaji aliambia shirika la habari la AP, kuwa miili hiyo ilipelekwa katika hospitali iliyo katibu na eneo la vita.
Waziri wa mambo ya ndani Arsen Avakov, amesema kuwa hapakuwa na majeruhi upande wa wanajeshi wa Ukraine.
Makabiliano yaliyozuka Jumatatu, yalianza baada ya wapiganaji wanaotaka kujitenga na Ukraine kuvamia uwanja wa ndege wa Sergei Prokofiev Donetsk mapema asubuhi.
Wakati huohuo,maafisa wa Ukraine wamedhibiti uwanja wa ndege mjini Donetsk mashariki mwa nchi hiyo huku idadi kubwa ya watu wakifariki. Hata hivyo, wandishi  walio nje ya kambi ya jeshi wanasikia milio ya risasi
Siku moja tu baada ya ushindi wa Rais mpya Petro Poroshenko, hali ya suitofahamu bado inaenea Mashariki mwa Ukraine.
Afisa mmoja wa serikali amesema kuwa operesheni dhidi ya wapiganaji hao itaendelea huku walinzi wa mipakani wakisema kuwa magari yenye wapiganaji waUk

No comments: