Tuesday 13 May 2014

Kurejea wakimbizi, mstari mwekundu kwa Palestina"

"Kurejea wakimbizi, mstari mwekundu kwa Palestina"Serikali halali iliyochaguliwa na wananchi wa Palestina inayoongozwa na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina HAMAS imesema kuwa, kurejeshwa wakimbizi wa Kipalestina kwenye ardhi zao za asili ni mstari mwekundu na suala hilo halihitajii mazungumzo ya aina yoyote. Muhammad al Mad houn Waziri wa Vijana, Michezo na Utamaduni wa serikali halali ya Palestina ameyasema hayoUkanda wa Ghaza wakati wa kuadhimisha kutimia miaka 66 ya kukaliwa kwa mabavu ardhi za Palestina na kuongeza kuwa, wananchi wa Palestina kamwe hawatafumbia macho hata chembe haki zao na wataendelea kufanya juhudi za kuhakikishakwamba kadhia ya wakimbizi wa Kipalestina inakuwa ya kimataifa. Waziri Mad houn ameongeza kuwa,  serikali yoyote itakayokuja madarakani inapasa kufungamana kikamilifu na haki zote za wananchi wa Palestina. Hivi sasa kuna Wapalestina zaidi ya milioni tano na nusu waliolazimika kuwa wakimbizi kutokana na hatua ya utawala wa Israel kuzikalia kwa mabavu ardhi za Wapalestina. Inafaa kuashiria hapa kuwa utawala ghasibu na bandia wa Israel ulitangazwa kuwepo kwake tarehe 14 Mei 1948 kwa uungaji mkono wa Uingereza.

No comments: