RIO DE JANEIRO, BRAZIL
WAKATI fainali za Kombe la Dunia zikiwa
zinakaribia kuanza, vioja mbalimbali vimeanza kuibuka kutokana na maombi
mbalimbali yanayowasilishwa na baadhi ya timu katika masharti ya
kushiriki fainali hizo.
Ronaldo kulindwa na mabaunsa sita
Shirikisho la Soka la Ureno limeomba walinzi sita
kwa ajili ya safari zao mbalimbali za kujiburudisha miili yao katika
fukwe za Copacabana na kwingineko. Kati ya walinzi wao, wanne watakuwa
na kazi ya kumlinda Mwanasoka Bora wa Dunia kwa sasa, Cristiano Ronaldo
peke yake wakati wengine watakuwa na kazi ya kulinda wachezaji wengine
na viongozi wa timu hiyo. Ronaldo, Lionel Messi na Neymar wanatarajiwa
kuwa mastaa wenye mvuto zaidi katika michuano hiyo kutokana na ubora wao
katika ligi mbalimbali za Ulaya.
Ufaransa wataka sabuni za maji
Katika hali ya kushangaza, Ufaransa ambao
wataongozwa na wakali kama Franck Ribery, Olivier Giroud, Karim Benzema
na wengineo wametoa madai ya kushtusha zaidi baada ya kudai kwamba
watataka sabuni za maji katika vyumba vya wachezaji wao na si sabuni za
vipande.
Uongozi wa mabingwa hao wa Kombe la Dunia mwaka
1998 wanataka vyumba vyao vyote vya hoteli watakayofikia jijini Sao
Paulo kuwekwa sabuni za maji na sio sabuni za vipande. Ufaransa pia
wanataka hoteli yao iwe na nyama ambazo zimechinjwa kihalali kwa sababu
wachezaji wao wengi ni Waislamu.
Akina Valencia wataka ndizi zao
Timu ya taifa ya Ecuador imeandika maombi yao ya
kutaka kila mchezaji wao apewe kikapu cha ndizi mbivu kutoka nchini kwao
Ecuador kila siku ya michuano hiyo. Kikosi chao kinachoongozwa na mkali
wa Manchester United, Antonio Valencia kinataka ndizi hizo zisafirishwe
kutoka katika ardhi ya kwao Ecuador kila siku. Ndizi mbivu ni chakula
maarufu kwa wanasoka wote duniani kwa ajili ya kurudisha sukari
iliyopotea mwilini kutokana na mazoezi mazito ya kila siku.
Algeria wataka Kurani kila chumba
Shirikisho la Soka la Algeria limetaka kila chumba
cha wachezaji pamoja na maofisa watakaoambatana na timu hiyo kuwekwa
vitabu vitakatifu vya dini ya Kiislamu, Kurani kwa ajili ya maombi yao
ya kila siku wakati watakapokuwa katika michuano hiyo. Kikosi chote cha
Algeria kitakuwa na wachezaji Waislamu. Hapana shaka baadhi ya wachezaji
wakubwa duniani wanaofuata imani ya Kiislamu ambao watakuwa katika
michuano hiyo wanaweza kuhitaji pia kuwekewa Kurani katika vyumba vya
hoteli zao. Wachezaji hao ni kama Mesut Ozil, Yaya Toure, Cheikh Tiote,
Samir Nasri na wengineo.
Australia wataka vyumba vya kahawa
No comments:
Post a Comment