Monday, 5 May 2014

Ronado Kuwekewa mabausa 6 kombe la dunia


 

RIO DE JANEIRO, BRAZIL
WAKATI fainali za Kombe la Dunia zikiwa zinakaribia kuanza, vioja mbalimbali vimeanza kuibuka kutokana na maombi mbalimbali yanayowasilishwa na baadhi ya timu katika masharti ya kushiriki fainali hizo.
Ronaldo kulindwa na mabaunsa sita
Shirikisho la Soka la Ureno limeomba walinzi sita kwa ajili ya safari zao mbalimbali za kujiburudisha miili yao katika fukwe za Copacabana na kwingineko. Kati ya walinzi wao, wanne watakuwa na kazi ya kumlinda Mwanasoka Bora wa Dunia kwa sasa, Cristiano Ronaldo peke yake wakati wengine watakuwa na kazi ya kulinda wachezaji wengine na viongozi wa timu hiyo. Ronaldo, Lionel Messi na Neymar wanatarajiwa kuwa mastaa wenye mvuto zaidi katika michuano hiyo kutokana na ubora wao katika ligi mbalimbali za Ulaya.
Ufaransa wataka sabuni za maji
Katika hali ya kushangaza, Ufaransa ambao wataongozwa na wakali kama Franck Ribery, Olivier Giroud, Karim Benzema na wengineo wametoa madai ya kushtusha zaidi baada ya kudai kwamba watataka sabuni za maji katika vyumba vya wachezaji wao na si sabuni za vipande.
Uongozi wa mabingwa hao wa Kombe la Dunia mwaka 1998 wanataka vyumba vyao vyote vya hoteli watakayofikia jijini Sao Paulo kuwekwa sabuni za maji na sio sabuni za vipande. Ufaransa pia wanataka hoteli yao iwe na nyama ambazo zimechinjwa kihalali kwa sababu wachezaji wao wengi ni Waislamu.
Akina Valencia wataka ndizi zao
Timu ya taifa ya Ecuador imeandika maombi yao ya kutaka kila mchezaji wao apewe kikapu cha ndizi mbivu kutoka nchini kwao Ecuador kila siku ya michuano hiyo. Kikosi chao kinachoongozwa na mkali wa Manchester United, Antonio Valencia kinataka ndizi hizo zisafirishwe kutoka katika ardhi ya kwao Ecuador kila siku. Ndizi mbivu ni chakula maarufu kwa wanasoka wote duniani kwa ajili ya kurudisha sukari iliyopotea mwilini kutokana na mazoezi mazito ya kila siku.
Algeria wataka Kurani kila chumba
Shirikisho la Soka la Algeria limetaka kila chumba cha wachezaji pamoja na maofisa watakaoambatana na timu hiyo kuwekwa vitabu vitakatifu vya dini ya Kiislamu, Kurani kwa ajili ya maombi yao ya kila siku wakati watakapokuwa katika michuano hiyo. Kikosi chote cha Algeria kitakuwa na wachezaji Waislamu. Hapana shaka baadhi ya wachezaji wakubwa duniani wanaofuata imani ya Kiislamu ambao watakuwa katika michuano hiyo wanaweza kuhitaji pia kuwekewa Kurani katika vyumba vya hoteli zao. Wachezaji hao ni kama Mesut Ozil, Yaya Toure, Cheikh Tiote, Samir Nasri na wengineo.
Australia wataka vyumba vya kahawa

No comments: