Sunday, 4 May 2014

Man city yapata matumaini ya kuchukua Ubingwa

Mancity yaweka hai matumaini ya ubingwa

Manchester city wameweka matumaini ya kutwaa ubinga wa ligi hai baada ya kuicharaza Everton 3-2 katika mchuano mgumu uliosakatwa ugani Goodison Park.

mancity-yaweka-hai-matumaini-ya-ubingwaMan City walijipa matumaini ya kutwaa ubingwa wa ligi ya Uingereza baada ya kuicharaza timu ya Everton. Man City sasa inaongoza ligi hiyo kwa wingi wa mabao.
Everton ilitangulia kufunga kupitia mchezaji Ross Barkeley katika dakika ya 11. Man City walisawazisha katika dakika ya 22 kupitia mshambuliaji matata Sergio Aguero. Edin Dzeko alipachika wavuni bao la pili na la tatu. Everton waliweza kupata bao la pili kupitia mchezaji Lukaku bali jitihada zao za kusawazisha hazikufua dafu.
Everton walitarajia kushinda na kujipa matumaini ya kufuzu kwa ligi ya mabingwa wa ulaya pamoja na kuwasaidia majirani wao Liverpool kunyakua ubingwa wa ligi ya Uingereza.

No comments: