Afisa mmoja aliuawa katika shambulizi la bomu mjini Cairo,huku watu wawili wakiuawa kwa kupigwa risasi katika mji wa bandari wa Alexandria wakati wafuasi wa aliyekuwa rais wa taifa hilo Mohammed Morsi walipokuwa wakikabiliana na wakaazi .
Wanamgambo wameimarisha mashambulizi yao dhidi ya vikosi vya usalama licha ya kuwepo kwa msako dhidi ya waislamu wenye itikadi kali na wanajeshi wa serikali.
Waandishi wanasema kuwa aliyekuwa kiongozi wa jeshi Abdel Fattah Al sisi ambaye mwaka uliopita alimuondoa madarakani Mohammed Morsi anatarajiwa kushinda kwa wingi wa kura.
No comments:
Post a Comment