Ripoti hiyo inabainisha kwamba malalamiko hayo
yaliletwa na kundi linalopinga ubaguzi la Kick It Out baada ya shabiki
wa Liverpool kudaiwa kutoa kauli ambazo zilionekana kuwa ni za kibaguzi.
Ba, ambaye alisema yeye binafsi hakusikia ubaguzi
huo, alifunga bao la kwanza wakati Chelsea walipoinyuka Liverpool mabao
2-0 na kuwatibulia kasi yao katika kuwania ubingwa wa Ligi Kuu England.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail, msemaji wa
Liverpool alisema: “Tunatambua kuhusu malalamiko yaliyoletwa na Kick It
Out na tupo kwenye uchunguzi wa jambo hilo.”
No comments:
Post a Comment