klabu yoyote ya Tanzania. Hivyo wasijisumbue.
Kauli hiyo ya Simba imekuja baada ya Azam FC kuwasajili Didier Kavumbagu na Frank Domayo wa Yanga ambao walikuwa wachezaji huru.
Klabu hiyo pia ilihusishwa na mipango ya
kuwasajili Tambwe na Mkude ili kuimarisha kikosi chake tayari kwa msimu
ujao wa Ligi Kuu Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika.
Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema;
“Tambwe na Mkude bado ni wachezaji wetu na hatuwauzi kwa klabu yoyote
hivi sasa. Kama kuna timu inawahitaji wajue hawapati kitu na hatuna muda
wa kuzungumza nao kwani hawa ni wachezaji wetu na tunahitaji mchango
wao katika timu.”
“Tunaweza kuwauza pengine nje ya nchi tena kwa dau
kubwa, kwa maana hatuwezi kukataa ofa nzuri kutoka nje ya nchi bila
sababu huko tunaweza kuwauza lakini siyo kwa klabu za humu ndani.”
Kamwaga alisema hawawezi kuwauza nyota hao kwa
klabu wanazoshindana nazo kwavile wanajua na wameona madhara yake. Hivyo
kama kuna timu ilipanga kuwasajili iandike maumivu. “Kila mchezaji ana
bei yake hapo, Tambwe na Mkude tunaweza kuwauza nje ya nchi tena kwa dau
kubwa, lakini siyo Tanzania tena kwa timu tunazoshindana nazo.”
Tambwe amebakiza mwaka mmoja wa mkataba wake kama
ilivyo kwa Mkude na ndiyo wachezaji wanaoibeba Simba katika mechi
mbalimbali za klabu hiyo.
No comments:
Post a Comment